Monday, September 17, 2012

Wadau mnamjua Armadillo?

Najua wengi mtashangaa lakini huyu ni katuni atakayetumika kulitangaza kombe la dunia litakalochezwa Brazil mwaka 2014 (Yaani 2014 FIFA World Cup Brazil) na ametangazwa kuwa balozi wa mashindano hayo jana kama chaguo la chama cha mpira wa miguu Brazil ambao ni wenyeji kamili wa mashindano hayo kupitia TV Globo kupitia kipindi chake cha soka kinachojulikana kama Fantastico.Ronaldo de Lima aliye mmoja wa wanakamati katika kamati ya maandalizi pamoja na Jerome Valke ambaye ni katibu mkuu wa FIFA wamefurahia kutangazwa huko kwa kikaragosi huyu(mascot) kuwakilisha mashindano hayo.
Armadillo ni mnyama mwenye asili ya Brazil ambaye amekaribia kabisa kupitoe (endangered specie) na jina lake la kisayansi ni Tolypeutes tricinctus
 

No comments:

Post a Comment