Thursday, September 20, 2012

Mayweather vs Manny Pacquiao pengine mwakani?!!

Baada ya Manny Pacquiao kukubali masharti ya Mayweather kwenye mgawanyo wa pesa mabingwa hawa wa kihistoria huenda wakapigana mwakani na kumaliza ubishi wa muda mrefu kwamba nani ni zaidi kati yao.Mayweather ameachiwa toka gerezani mwezi uliopita na amekua mkimya sana na Pacman anajiandaa na pambano la kukata na shoka Dec 8 dhidi ya bingwa mpya wa dunia Marquez ambapo atakua anapigana na Marquez kwa mara ya nne ingawa huko nyuma kumekua na utata kuhusu waamuzi waliotumika na uhalali wa matokeo wa mapambano kati yao.Iwapo Pacquiao atashinda itaongeza hamasa la pambano kati yake na Mayweather.Pacman amekubali mgawanyo wa malipo kati yao kuwa asilimia 55 kwa asilimia 45 kama alivyotaka Maywether mwanzoni.

No comments:

Post a Comment