Saturday, September 29, 2012

Lewis Hamilton kuelekea Mercedes msimu ujao

Imethibitika kwamba Lewis Hamilton ataihama timu yake ya McLaren msimu ujao na hapo jana timu hiyo imemtangaza raia wa Mexico anayeendeshea magari ya langalanga ya timu ya Sauber kwa sasa Sergio Perez kama mbadala wake msimu ujao.
Martin Whitmarsh ambaye ni Afisa Mtendaji Mkuu(CEO) wa McLaren Racing ametangaza jana akielezea kufurahishwa kwake na ujio wa bwana Perez kwenye timu yake msimu ujao na kusisitiza hakuna dereva aliye mkubwa kuzidi timu.

No comments:

Post a Comment