Tuesday, September 11, 2012

Mbuyu Twite na Yondani ruksa kuchezea Yanga

Baada ya kamati ya sheria,maadili na hadhi ya wachezaji kuridhia usajili wa wachezaji hawa wawili kuwa halali wamepitishwa rasmi kuichezea Yanga kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara,Vodacom Premier League inayotarajiwa kuanza siku ya jumamosi tarehe 15/09/2012.Kwa usajili ya Mbuyu Yanga inatakiwa kuilipa Simba dola 32,000 inazosemekana Wekundu wa Msimbazi walimpatia mchezaji huyo huko Kigali.Wachezaji hawa kwenda Yanga kumewaumiza sana mahasimu wao Simba baada ya Twite kuwabeza na Yondani kuhamia Yanga akitokea Simba.

No comments:

Post a Comment