Sunday, September 23, 2012

Super Sunday-Manchester City vs Arsenal

Mara ya Mwisho Arsenal kwenda Etihad ni Manchester City ndo waliibuka na ushindi wa goli 1 - 0 na goli lilifungwa na kiungo mahiri wa Manchester City David Silva katika dakika ya 53.Hii ilikua Desemba mwaka jana wakati Arsenal ikisemekana kuwa na wakati mgumu baada ya kuanza msimu uliopita vibaya na ilicheza chini ya kiwango huku ikishindwa kukaa na mpira na kucheza pasi nyingi za karibu na ndefu kama ilivyo kawaida ya timu hiyo ya London.Lakini msimu mmoja baadae Arsenal inajigamba kuwa timu ya ulinzi bora msimu huu Uingereza na pengine Ulaya nzima ikiwa imeruhusu goli moja tu,rekodi ambayo haijafikiwa na timu yoyote katika madaraja yote manne ya ligi za mpira katika Taifa la Uingereza.
Manchester City wakiwa wenyeji,mabingwa watetezi na pia wakiwa na kumbukumbu ya kipigo walichokipata Emirates mwishoni mwa msimu uliopita naamini watataka kurudisha heshima leo wakiwa nyumbani kwao pamoja na kuanza vibaya mechi za klabu bingwa Ulaya kwa kufungwa na Barcelona katikati ya wiki.Pamoja na kufungwa walionyesha kiwango bora kwa kuweza kucheza kwa upinzani mkubwa dhidi ya Real Madrid.
Hakuna shabiki wa Arsenal leo asiyetaka kuimba nyimbo za kuwakejeli Samir Nasri,Gael Clichy na hata Kolo Toure baada ya ushindi katika mechi hiyo itakayoanza saa 12 kamili kwa saa za Afrika mashariki.
Tuache maneno tusubiri muda wa game wandugu.

No comments:

Post a Comment