Saturday, September 29, 2012

Sijui wabongo mnaijua Ryder Cup?


Ryder Cup ni kikombe mashindano ya tennis yanayochezwa kila baada ya miaka miwili kati ya timu ya Marekani dhidi ya timu ya mataifa ya Ulaya na husimamiwa kwa pamoja kati ya chama cha mchezo wa golf kiprofesheno cha Marekani (PGA of America) na kile kinachosimamia mchezo huo kiprofesheno Ulaya PGA European Tour.Washiriki hupatikana kwa viwango vyao na wachache huchaguliwa na Nahodha wa kila timu.
Cha kushangaza mwaka huu kwenye mashindano haya ni uamuzi wa jana wa Nahodha wa timu ya Marekani kutomshirikisha katika hatua za Mwisho Tiger Woods ambaye siku zilizotangulia alishindwa.Na hii ni pamoja na kwamba Marekani inaongoza ikiwa na advantage ya 5-3 ambapo wana nafasi kubwa ya kushinda kikombe cha mwaka huu.Nahodha huyo Davis Love III amesema amefanya hivyo kumpumzisha baada ya siku mbili za mwanzo akielezea kiwanja wanachotumia cha Medinah Country Club,Medinah,Illinois kuwa ni kigumu na hangependa wachezaji wa timu yake kuchoka sana kwa kucheza mechi 5 katika kipindi cha mashindano hayo.Mashindano hayo yataendelea kesho baada ya mapumziko ya leo.

No comments:

Post a Comment