Mtanisamehe wadau wote maana nilipoteza password ya akaunti yangu hiyo kushindwa kuweka updates na kuwajuza yanayojiri katika ulimwengu wa michezo.Kuanzia sasa nitajitahidi kufanya hivyo...
Mwenyekiti
MICHEZO DUNIANI
Sunday, July 13, 2014
Saturday, March 30, 2013
Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara
Kabla ya matokeo ya mechi za March 30.
Rank
|
Teams
|
Played
|
Wins
|
Draw
|
Lost
|
GD
|
Points
|
1
|
Young Africans
|
20
|
15
|
3
|
2
|
25
|
48
|
2
|
Azam FC
|
21
|
13
|
4
|
4
|
20
|
43
|
3
|
Simba SC
|
20
|
9
|
7
|
4
|
11
|
34
|
4
|
Kagera Sugar
|
21
|
9
|
7
|
5
|
5
|
34
|
5
|
Mtibwa Sugar
|
21
|
8
|
8
|
5
|
4
|
32
|
6
|
Coastal Union
|
21
|
8
|
8
|
5
|
4
|
32
|
7
|
Ruvu Shooting
|
20
|
8
|
5
|
7
|
2
|
29
|
8
|
JKT Oljoro
|
21
|
6
|
7
|
8
|
-3
|
25
|
9
|
Mgambo Shooting
|
21
|
7
|
3
|
11
|
-6
|
24
|
10
|
JKT Ruvu
|
20
|
6
|
4
|
10
|
-13
|
22
|
11
|
Prisons FC
|
21
|
4
|
8
|
9
|
-9
|
20
|
12
|
Police Moro
|
21
|
3
|
8
|
10
|
-10
|
17
|
13
|
Toto African
|
21
|
3
|
8
|
10
|
-12
|
17
|
14
|
African Lyon
|
21
|
4
|
4
|
13
|
-18
|
16
|
Matokeo Ligi kuu ya Ujerumani-Bundesliga Matchday 27
Leo Bayern Munich wameisogelea zaidi ndoto yao ya kuweka historia huku wakikaribia ubingwa wa ligi ya Ujerumani mashuhuri kama Bundesliga kwa kuwapiga Hamburg kwa goli 9 - 2.Pichani juu Claudio Pizzaro akifunga mojawapo ya magoli hayo 9.
Stuttgart 1 - 2 Dortmund
Freiburg 2 - 0 Munchegladbach
Dusseldorf 1 - 4 Leverkusen
Augsburg 0 - 2 Hannover
Mainz 1 - 1 Bremen
Schalke 04 3 - 0 Hoffenheim
FC Bayern 9 - 2 Hamburg
Matokeo ligi kuu Uingereza Matchweek 31
Manchester United wameendeleza wimbi la ushindi na kujikita kwenye usukani wa Ligi Kuu ya Uingereza(EPL) baada ya ushindi wa goli moja lilitokana na kazi nzuri ya Robin van Persie na kumsabisha Titus Bramble wa Sunderland ajifunge kama inavyoonekana pichani juu.
Sunderland 0 - 1 Man Utd
Bramble 27 og
Manchester City leo nao hawakubaki nyuma kushikilia vizuri zaidi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kwa kutoa adhabu kali ya magoli 4 kwa Newcastle Utd.Pichani juu Silva akifunga goli la pili.
Man City 4 - 0 Newcastle
Tevez 41
Silva 45+2
Kompany 56
Perch 69 og
Chelsea wamekutana na kisiki cha Southampton leo na wakala kipigo cha goli 2 - 1 ugenini.Pichani juu Rodriguez akimalizia mambo dhidi ya Cech.
Southampton 2 - 1 Chelsea
Rodriguez 23 John Terry 33
Rickie Lambert 35
Na the Gunnerz leo waliamka toka usingizini na kuwaweka mkiani mwa EPL timu ya Reading kwa kuwafunga magoli manne huku wakitawala sehemu kubwa ya mchezo huku Kirean Gibbs akicheza mechi yake ya 100 kwa timu hiyo ya kaskazini ya London.Mnamo dakika ya saba ya mchezo uwanja wote ulisimama na kupiga makofi kama heshima ya kumbukumbu ya mchezaji namba saba wa zamani anayekumbukwa zaidi na aliyefariki kwa ugonjwa wa kansa (Hodgkin's Lymphoma) mwaka 2001 maarufu kama Rocky 7 (David Rocastle)
Arsenal 4 - 1 Reading
Gervinho 11
Carzola 48
Giroud 68
Arteta 77 pen
Matokeo ya michezo mingine ni kama ifuatavyo:
Swansea 1 - 2 Tottenham
West Ham 3 - 1 West Brom
Wigan 1 - 0 Norwich
Sunderland 0 - 1 Man Utd
Bramble 27 og
Manchester City leo nao hawakubaki nyuma kushikilia vizuri zaidi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kwa kutoa adhabu kali ya magoli 4 kwa Newcastle Utd.Pichani juu Silva akifunga goli la pili.
Man City 4 - 0 Newcastle
Tevez 41
Silva 45+2
Kompany 56
Perch 69 og
Chelsea wamekutana na kisiki cha Southampton leo na wakala kipigo cha goli 2 - 1 ugenini.Pichani juu Rodriguez akimalizia mambo dhidi ya Cech.
Southampton 2 - 1 Chelsea
Rodriguez 23 John Terry 33
Rickie Lambert 35
Na the Gunnerz leo waliamka toka usingizini na kuwaweka mkiani mwa EPL timu ya Reading kwa kuwafunga magoli manne huku wakitawala sehemu kubwa ya mchezo huku Kirean Gibbs akicheza mechi yake ya 100 kwa timu hiyo ya kaskazini ya London.Mnamo dakika ya saba ya mchezo uwanja wote ulisimama na kupiga makofi kama heshima ya kumbukumbu ya mchezaji namba saba wa zamani anayekumbukwa zaidi na aliyefariki kwa ugonjwa wa kansa (Hodgkin's Lymphoma) mwaka 2001 maarufu kama Rocky 7 (David Rocastle)
Arsenal 4 - 1 Reading
Gervinho 11
Carzola 48
Giroud 68
Arteta 77 pen
Matokeo ya michezo mingine ni kama ifuatavyo:
Swansea 1 - 2 Tottenham
West Ham 3 - 1 West Brom
Wigan 1 - 0 Norwich
Thursday, March 14, 2013
Saturday, March 9, 2013
Marakana yafurika
Pichani juu mojawapo ya viwanja vitakavyotumika katika Kombe la Dunia Brazil mwakani ukiwa umefurika maji baada ya mvua kubwa zinazoendelea Brazil.Uwanja huu unatazamiwa kutumiwa kwenye mechi ya kirafiki Juni 2 kati ya Brazil na Uingereza.Umewahi kusemwa kuwa uwanja mkubwa zaidi duniani na kwa sasa unafanyiwa ukarabati ambapo paa limeezuliwa upande mmoja,viti viliondolewa na sasa umebainika una tatizo la kufurika maji hii ikiwa mara ya pili hili kurokea.Ni changamoto kubwa kwa maandalizi ya kombe la dunia mwakani ambapo ulitazamiwa kutumika kwenye ufunguzi na mechi ya mwisho/fainali ya mashindano
Golikipa afungwa miaka 22 jela kwa kumuua mpenzi wake
Mmojawapo wa waliokuwa magolikipa bora zaidi kwenye ligi kuu ya Brazil na aliyekua nahodha wa timu ya Flamengo ya huko inayoshiriki Ligi kuu ya Brazil juzi alihukumiwa kifungo cha miaka 22 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mpenzi wake wa zamani na kisha kuukatakata mwili wake na kuwalisha mbwa.
Bruno Fernandes de Souza alikuwa katika nafasi nzuri kuitwa kwenye timu ya taifa ya Brazil na pia kusajiliwa kwa mkataba mkubwa na timu ya AC Milan wakati siri za mauaji haya ya kutisha zilipoanza kuibuka Brazil.Alituhumiwa kumuua mpenzi wake aliyekua pia mwanamitindo nchini humo baada ya kumlaghai na kumualika katika shamba lililo katika jimbo la Minas Gerais ambako binti huyo aliuawa na kisha kukatwakatwa vipande vipande na maiti yake kulishwa mbwa waliokuwa maeneo hayo.Maiti yake haijapatikana hadi leo hii.
Mwanamitindo Eliza Samudio pichani juu aliwahi pia kutekwa siku za nyuma akiwa na ujauzito wa Bruno na kushawishiwa pamoja na kulazimishwa kuitoa mimba hiyo ambapo alikataa na kupeleka mashitaka polisi.Wakati wa kesi hiyo hakuonekana na katika uchunguzi ndo yalipoibuka haya ya mauaji ya kutisha ambapo Bruno aliwashirikisha baadhi ya ndugu zake,marafiki wa karibu,mke wake wa zamani na hata mmojawapo wa wachumba zake.
Bruno amepewa hukumu ndogo kwa sababu ya kushirikiana kwake na polisi na pia kutubu kushiriki mauaji hayo mahakamani ingawa amekua akisisitiza kwamba mrembo huyo aliuawa kwa bahati mbaya na rafiki yake na kwamba yeye alishiriki zaidi katika kumshawishi kwenda katika shamba alipoikuta mauti yake na pia katika kuupoteza mwili baada ya kifo kutokea.
Bruno Fernandes de Souza alikuwa katika nafasi nzuri kuitwa kwenye timu ya taifa ya Brazil na pia kusajiliwa kwa mkataba mkubwa na timu ya AC Milan wakati siri za mauaji haya ya kutisha zilipoanza kuibuka Brazil.Alituhumiwa kumuua mpenzi wake aliyekua pia mwanamitindo nchini humo baada ya kumlaghai na kumualika katika shamba lililo katika jimbo la Minas Gerais ambako binti huyo aliuawa na kisha kukatwakatwa vipande vipande na maiti yake kulishwa mbwa waliokuwa maeneo hayo.Maiti yake haijapatikana hadi leo hii.
Mwanamitindo Eliza Samudio pichani juu aliwahi pia kutekwa siku za nyuma akiwa na ujauzito wa Bruno na kushawishiwa pamoja na kulazimishwa kuitoa mimba hiyo ambapo alikataa na kupeleka mashitaka polisi.Wakati wa kesi hiyo hakuonekana na katika uchunguzi ndo yalipoibuka haya ya mauaji ya kutisha ambapo Bruno aliwashirikisha baadhi ya ndugu zake,marafiki wa karibu,mke wake wa zamani na hata mmojawapo wa wachumba zake.
Bruno amepewa hukumu ndogo kwa sababu ya kushirikiana kwake na polisi na pia kutubu kushiriki mauaji hayo mahakamani ingawa amekua akisisitiza kwamba mrembo huyo aliuawa kwa bahati mbaya na rafiki yake na kwamba yeye alishiriki zaidi katika kumshawishi kwenda katika shamba alipoikuta mauti yake na pia katika kuupoteza mwili baada ya kifo kutokea.
Subscribe to:
Posts (Atom)