Saturday, March 30, 2013

Matokeo ligi kuu Uingereza Matchweek 31

Manchester United wameendeleza wimbi la ushindi na kujikita kwenye usukani wa Ligi Kuu ya Uingereza(EPL) baada ya ushindi wa goli moja lilitokana na kazi nzuri ya Robin van Persie na kumsabisha Titus Bramble wa Sunderland ajifunge kama inavyoonekana pichani juu.

                                         Sunderland    0   -    1 Man Utd
                                                                           Bramble 27 og


Manchester City leo nao hawakubaki nyuma kushikilia vizuri zaidi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kwa kutoa adhabu kali ya magoli 4 kwa Newcastle Utd.Pichani juu Silva akifunga goli la pili.

                                    Man City       4     -      0     Newcastle
                                    Tevez 41
                                    Silva 45+2
                                    Kompany 56
                                    Perch 69 og

Chelsea wamekutana na kisiki cha Southampton leo na wakala kipigo cha goli 2 - 1 ugenini.Pichani juu Rodriguez akimalizia mambo dhidi ya Cech.

                                     Southampton   2   -     1    Chelsea
                                     Rodriguez 23                    John Terry 33
                                     Rickie Lambert 35


Na the Gunnerz leo waliamka toka usingizini na kuwaweka mkiani mwa EPL timu ya Reading kwa kuwafunga magoli manne huku wakitawala sehemu kubwa ya mchezo huku Kirean Gibbs akicheza mechi yake ya 100 kwa timu hiyo ya kaskazini ya London.Mnamo dakika ya saba ya mchezo uwanja wote ulisimama na kupiga makofi kama heshima ya kumbukumbu ya mchezaji namba saba wa zamani anayekumbukwa zaidi na aliyefariki kwa ugonjwa wa kansa (Hodgkin's Lymphoma) mwaka 2001 maarufu kama Rocky 7 (David Rocastle)

                                    Arsenal      4         -        1      Reading
                                    Gervinho  11
                                    Carzola 48
                                    Giroud 68
                                    Arteta 77 pen


Matokeo ya michezo mingine ni kama ifuatavyo:

                              Swansea      1    -     2        Tottenham
                              West Ham    3    -    1        West Brom
                              Wigan          1    -     0        Norwich 
                                   







No comments:

Post a Comment