Monday, September 10, 2012

Andy Murray ashinda Granda Slam ya kwanza

Andy Murray ameshinda mashindano makubwa (Grand Slam) kwa mara ya kwanza katika maisha yake usiku wa kuamkia leo kwenye mashindano ya Wazi ya Marekani (US Open) hii ikiwa ni mara ya tano kwake kucheza fainali kwenye Grand Slam.Kati ya mashabiki waliokuwa uwanjani ni Muigizaji maarufu aliyewahi kuigiza kama James Bond bwana Sean Connery na kocha wa Manchester United Alex Ferguson waliokuwa wakimshabikia.Fainali hii alikutano na Novac Djokovic wa Serbia huko New York kwa seti 7-6,7-5,2-6,3-6,6-2.Serena Williams alishinda mashindano hayo kwa wanawake jana ikiwa mara yake ya nne kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment