Saturday, September 29, 2012

Chelsea yashinda Battle of London

Kwa mara ya kwanza Arsenal wamepoteza mchezo msimu huu walipokutana na Chelsea mapema leo kwenye uwanja wa Emirates matokeo haya yakiwa ni magoli yaliyotokana na mipira ya adhabu.Arsenal walionyesha udhaifu katika kulinda dhidi ya mipira ya adhabu na pengine lilikuwa kosa kumchezesha Laurent Koscielny leo badala ya Per Metersacker.
Chelsea ambao wamezidi kujiongezea kasi ya kuuelekea ubingwa wa Ligi msimu huu walitawala zaidi nafasi ya kiungo na pengine pengo la Abou Diaby lilikuwa dhahiri kwa Arsenal.
Magoli yalifungwa na Fernando Torres na Juan Mata kwa Chelsea na lile la Arsenal kufungwa na Gervinho.Matokeo ya mwisho Arsenal 1 - 2 Chelsea.mechi nyingine za ligi ya Uingereza EPL zinaendelea kwa sasa.

No comments:

Post a Comment