Sunday, September 23, 2012

Arsenal yabeba pointi Etihad


Arsenal hapo jana imecheza mechi yake ngumu ya kwanza na matokeo ya mechi yalikuwa suluhu ya goli
1 - 1  magoli yote mawili yakifungwa na ma-centre half wa timu hizo katika mechi iliyojaa ufundi katikati ya uwanja huku kiungo wa Arsenal toka Hispania Santiago Carzola akitawala mapambano hayo.Arsenal walionekana kutawala sehemu kubwa ya mchezo na Arsene Wenger amesema anaamini mechi hii inaonyesha mwanga wa uwezo wa timu yake na pengine itawaongezea imani kwamba wanaweza kufanya mambo makubwa msimu huu.Timu zote mbili zina mengi ya kujilaumu kwa kutoshinda mchezo wa jana lakini naamini Arsenal watajilaumu zaidi kutokana na Gervinho kupata  nafasi za wazi zaidi na kuzipoteza kizembe.Timu nyingi zimeenda Etihad na kutoka vichwa chini na kwa Arsenal kuchukua pointi ni matokeo mazuri sana kwao.Arsenal imeendeleza rekodi yake nzuri katika ulinzi ya kutofungwa msimu huu na pia imeruhusu magoli mawili tu msimu huu.
Katika mechi zingine kwenye ligi ya Uingereza weekend iliyopita matokeo yalikuwa.

Jumamosi 22/09/2012
Chelsea 1 - 0 Stoke
Southampton 4 - 1 Aston Villa
West Brom 1 - 0 Reading
West Ham 1 - 1 Sunderland
Wigan 1 - 2 Fulham
Swansea 0 - 3 Everton

Jumapili 23/09/2012

Tottenham 2 - 1 QPR
Newcastle 1 - 0 Norwich
Liverpool 1 - 2 Man Utd


No comments:

Post a Comment