Friday, August 31, 2012

Atletico de Madrid washinda European Super Cup

Hat-trick ya kipindi cha kwanza ya Radamel Falcao pamoja na nyongeza ya bao moja lililofungwa na Miranda kipindi cha pili yalitosha kuwapa ushindi wa goli 4-1 Atletico de Madrid dhidi ya Chelsea katika uwanja wa Stade Louis II dakika chache zilizopita.Kwa maana hii Atletico wataliwakilisha bara la Ulaya katika mashindano ya Klabu Bingwa ya Dunia katika msimu huu.Chelsea ilijipatia bao la kufutia machozi dakika ya 75 kupitia kwa Gary Cahill.

No comments:

Post a Comment