Thursday, August 30, 2012

UEFA Super cup leo Usiku (Chelsea vs Atletico Madrid)

Hii inatazamiwa kuwa leo usiku pale Stade de Louis II,mjini Monaco ambapo Chelsea ambao ni mabingwa wa Kombe la Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League) watakabana koo na Atletico Madrid ambao ni mabingwa wa Kombe la Europa League.Mshindi wa mechi hii huwa anapata nafasi ya kuliwakilisha bara la Ulaya kwenye mashindano ya klabu bingwa duniani.
Mechi itaanza kuchezwa saa 2 na dakika 45 kwa saa za Monaco.Hii itakua saa 3 na dakika 45 usiku kwa saa za Afrika Mashariki

No comments:

Post a Comment