Wednesday, August 29, 2012

Mbuyu Twite kuwasili leo

Habari rasmi zenye uthibitisho wa uongozi wa Young Africans SC ni kwamba Mbuyu Twite ambaye ni beki raia wa Rwanda mwenye asili ya DRC atawasili leo na kujiunga na wenzake kabla ya mchezo wa kirafiki kati ya Yanga na Coastal Union siku ya Jumamosi.Mchezaji huyu anatazamiwa kupata mapokezi makubwa hasa ukichukuliwa usajili wake uligubikwa na mashindano makubwa kati ya Yanga na wapinzani wao wakubwa Simba.

No comments:

Post a Comment