Thursday, August 30, 2012

Iniesta mchezaj bora Ulaya

Andreas Iniesta ametangazwa jana kuwa mchezaji bora wa mwaka Ulaya baada ya kupigiwa kura kuwa bora zaidi katika bara hilo na waandishi wa habari za michezo toka nchi wanachama wa chama cha mpira barani Ulaya (UEFA).Kiungo huyo wa timu ya soka ya Barcelona na pia tima ya soka ya taifa ya Hispania ameshinda kombe la dunia pamoja na lile la Ulaya akiwa na timu yake ya taifa ambapo mashindano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya lililopita liliisha akichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mashindano baada ya kucheza mechi zote ilizoshiriki timu yake.Iniesta pia ana rekodi ya kucheza zaidi ya mechi 50 za La Liga mfululizo bila timu yake kufungwa.Mchezaji huyo aliwashukuru wachezaji wenzake wa timu zote mbili na kuwakaribisha kushiriki tuzo yake hiyo.

No comments:

Post a Comment