Sunday, August 26, 2012

Madrid waumizwa na jirani zao Getafe

Real Madrid wameaibishwa na jirani zao Getafe katika mechi yao ya pili ya msimu mpya wa La Liga huku ikiwa ni mechi ya pili mfululizo kupoteza baada ya kufungwa na Barcelona katikati ya wiki katika mcheza wa kugombea Spanish Supercup.Getafe wameibuka na ushindi wa magoli 2-1 na kuwaweka pabaya Real Madrid katika harakati zao za kutetea ubingwa wa La Liga ambapo hadi sasa wameachwa pointi 5 na Barcelona ambao wamekuwa wapinzani wao wakubwa katika kugombea kombe hilo siku za karibuni.

No comments:

Post a Comment