Monday, August 20, 2012

Mo Farah uso kwa uso na Haile Gebrlselassie

Hii inatazamiwa kutokea huko Newcastle mwezi ujao tarehe 16 kwenye Mashindano ya Nusu Marathon ya Newcastle yanayojulikana kama Bupa Great North Run ambapo wakali hawa wanatazamiwa kukutana huku Mohamed Farah,Muingereza mwenye asili ya Somalia akitazamiwa kuwa Raia wa kwanza wa Uingereza kukimbia nusu marathoni ndani ya saa moja(Dakika 60) au pungufu hasa akiwa ndani ya ardhi ya Uingereza.Bingwa huyu wa mita 5000 na mita 10,000 kwenye mashindano ya Olimpiki yaliyomalizika huko London hivi karibuni amewahi kukimbia Nusu Marathon kama mshindani mara moja tu katika mashindano ya marathon ya New York yaliyopita ambapo alishinda akitumia saa 1:00:23 atakuwa anakabiliana na Gebrsellasie mwenye rekodi bora ya dakika 58:55 na aliyeyashinda mashindano hayo kwa muda wa dakika 59:33 mwaka juzi (2010)

No comments:

Post a Comment