Monday, August 20, 2012

USAJILI ARSENAL

Habari za kuaminika zimesambaa kupitia vyombo mbali mbali vya habari vikiongelea usajili wa Arsenal ambapo inasemekana katika wiki inayokuja Arsene Wenger amejipanga kutangaza usajili wa wachezaji watatu wa kukata na shoka.Wachezaji hao ni Nuri Sahin anayechukuliwa kwa mkopo toka Real Madrid huku habari zikidai mkopo umepita na unasubiri tu kutangazwa.

Wakati huo huo kiungo mkabaji wa Renne ya Ufaransa pamoja na timu ya taifa ya Ufaransa Yann M'villa anasemeka kuwa atafika London wiki hii kwa ajili ya uchunguzi wa afya na makubaliano ya Mwisho na Gunners.

Pia huko Hispania Fernando Llorente hakucheza mechi ya ufunguzi wa ligi ya huko kwa timu yake ya Athletic Bilbao na anasemekana kuwa katika mlango wa kuhama akihusishwa pia na kutua Emirates wiki ijayo.

Timu ya AC Milan inasemekana kuongeza kasi yake katika kumhamishia Arsenal beki wake wa kati Philipe Mexes ambaye amekua mkaidi kwa timu hiyo katika mpango wa kubadilishana wachezaji kwa kumjikua Nicklaus Bendtner ambaye ametamka wazi kwamba hataki tena kuichezea Arsenal.
Ntajitahidi kuwajuza pindi nipatapo habari. 

Katika hali ya kushangaza Tottenham wameulizia uwezekano wa kumsajilia Marouane Chamakh kwa mkopo toka Arsenal.Timu hzo ni mahasimu wakubwa huko North London.

No comments:

Post a Comment