Thursday, August 30, 2012

Michael Schumacker kushiriki Grand Prix ya 300

Michael Schumacker atashiriki mashindano ya 300 ya magari ya langa langa (Formula One Racing) siku ya jumapili katika mzunguko au circuit anayoiita sebuleni kwake kwani Belgian Grand Prix itafanyikia kwenye uwanja wa Spa ambapo mwendesha magari huyu bingwa mara saba wa dunia aliendesha kwa mara ya kwanza kabisa mwaka 1991 na pia ambapo alishinda kwa mara ya kwanza pia mwaka uliofuata.Wakati akishiriki Mwingereza Lewis Hamilton mwenye pointi 117 atakua anapambana kupata ushindi na kupunguza gap la point na anayeongoza mashindano ya dunia mwaka huu huku kukiwa na mabishano ndani ya timu ya McLaren baada ya mwingereza mwenzake Jenson Button(pointi 76) mwenye nafasi finyu ya kupata ubingwa wa dunia mwaka huu kutamka kwamba hatamsaidia mwenzake kufanya vyema zaidi kwenye mashindano ya kuwania ubingwa wa dunia mwaka huu.Fernando Alonso anaongoza mashindano ya kuwania ubingwa wa dunia akiwa na pointi 164

No comments:

Post a Comment