Wednesday, August 22, 2012

UMEPATA KUMSIKIA FABRICE OLINGA?!

Huyu ni kinda aliyeweka rekodi ya kuwa mchezaji mdogo kabisa kuwahi kufunga goli katika ligi kuu ya Hispania La Liga.Kijana toka Cameroon na anayeichezea Malaga ya Hispania alifunga goli hilo la ushindi dhidi ya Celta Vigo na ni matunda ya malezi mazuri ya Samuel Eto'o Foundation ndugu zangu.Alifunga goli hilo dakika 6 kabla ya mpira kwisha na Malaga wamemtunuku kwa kumuweka kwenye listi yao ya wachezaji watakaocheza Europa League.Alifunga akiwa na umri wa miaka 16 na siku 98.

No comments:

Post a Comment