Tuesday, August 21, 2012

JACK WILSHERE KUANZA MAZOEZI NDANI YA WIKI 4

Habari za kuaminika toka vyanzo mbalimbali ndani ya timu ya Arsenal vimesemekana kuthibtisha kwamba kiungo mdogo na mahiri wa timu hiyo na timu ya taifa ya Uingereza Jack Wilshere ambaye alikuwa majeruhi msimu mzima uliopita baada ya kuumia katika mechi za kirafiki kabla ya msimu kuanza huenda akaanza mazoezi mazito ndani ya wiki 4 zijazo na hivyo kurudi uwanjani.Hii itasaidia sana timu hiyo yenye mafanikio zaidi katika jiji la London na itakuwa kama usajili mpya.
Tovuti ya Arsenal imethibitisha pia kwamba mchezaji huyo anatazamiwa kurudi uwanjani akiwa pamoja na wachezaji wengine wa Arsenal kama Bacary Sagna,Tomas Rosicky na pia Emmanuel Frimpong.

No comments:

Post a Comment